Maombi yenye nguvu Maana ya Maombi: Maana ya maombi ni kusema na Mungu au kuhitaji msaada toka kwa Mungu. Isaya 43:26, Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako. Unikumbushe – Mungu anaposema tumkumbushe hana maana kuwa amesahau. Hapana. Ila anataka kuona moyoni umeweka nini. Ndiyo maana aliwaambia wana wa Israel kuwa “Niliwazungusha makusudi ili nione mioyoni mwenu mna nini.” Ndiyo maana tunatakiwa kuliweka Neno la Bwana mioyoni mwetu. Zab 119:10 Tuhojiane – Ni jambo la kumshukuru Mungu anayetupatia nafasi ya kueleza mambo yetu, kero zetu na shida zetu kwake kwa kuhojiana naye ili tupate kupewa haki zetu. Haki zetu: Katika Biblia ziko haki zetu nyingi sana ambazo Mungu wetu ametuahidi. Lakini bahati mbaya nyingi hatuzijuwi. Inatubidi kusoma Biblia kwa bidii ili Neno lake Kristo likae kwa wingi ndani yetu. Biblia ina mistari 31,173. Hebu jipime uone, wewe unaijua mingapi? Dan 9:1 – Daniel katika wakati wake alisoma kitabu alichokuwa ameandika n...
KUOKOLEWA KWA NEEMA Na Askofu Mkuu Zakaria Kakobe. Watu wanaosema kwamba haiwezekani kuokoka duniani, wanasema hivyo, kwa sababu hawajui kwamba tunaokolewa kwa neem a tu! Biblia inasema katika WAEFESO 2:8-9, “kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu (yaani zawadi kutoka kwa Mungu); wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu”. Tunasoma pia katika YOHANA 1:16, “Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema”. Iko siri kubwa iliyofichika katika maana ya neno, “Neema”.Kama sisi sote tungefahamu jinsi tunavyookolewa kwa neema, na jinsi tunavyopokea neema juu ya neema; kwa hakika, hakuna mtu hata mmoja ambaye angekwenda kwenye mateso ya moto wa milele. Wote tungekwenda mbinguni kirahisi sana, kwa kuwa tunaingia mbinguni, kwa neema tu; na Shetani asingepata mtu wa kukaa naye motoni, ila malaika zake tu, maana moto wa milele haukutengenezwa kwa ajili ya wanad...
Comments
Post a Comment